Taswira ya tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi katika tamthilia ya Kiswahili: Mfano wa Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi
Keywords:
tamthiliaAbstract
Makala haya yanachunguza tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na utamaduni wa kiafrika zilizotumiwa kiubunifu na waandishi katika utunzi wa tamthilia ya Kiswahili. Makala yanabainisha tanzu na tamaduni za kiafrika husika katika tamthilia za Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi na kufafanua mbinu walizozitumia watunzi katika kusababisha na kuibua maana ya ndani ya kazi zao kupitia kwa ejenzi wa taswira za kimaana. Makala haya vilevile yanashughulikia taswira zinazojengwa na tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na tamaduni za kiafrika zilizotumika katika utunzi wa tamthilia ya Kiswahili. Tamthilia nne za Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi zimehakikiwa kwa misingi ya nadhadharia za Uhistoria mpya iliyoasisiwa na Greenblat na na nadharia ya Mwingilianomatini iliyoasisiwa na Julian Kristeva. Tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na tamaduni za kiafrika zilizotumiwa katika utunzi wa tamthilia zetu teule zilibainiswa na kisha tukazihakiki kubaini taswira zinazojengwa kupitia kwa matumizi ya aina hiyo katika kujenga dhamira za mwandishi na umbo zima la tamthilia ya Kiswahili.
Downloads
Published
How to Cite
Issue
Section
This open-access article is distributed under a Creative Commons Attribution (CC-BY-NC-SA) license.
You are free to: Share — copy and redistribute the material in any medium or format.
Adapt — remix, transform, and build upon the material for any purpose, even commercially. The licensor cannot revoke these freedoms as long as you follow the license terms.
Under the following terms:
Attribution — You must give appropriate credit, provide a link to the license, and indicate if changes were made. You may do so in any reasonable manner, but not in any way that suggests the licensor endorses you or your use.
No additional restrictions You may not apply legal terms or technological measures that legally restrict others from doing anything the license permits.